Isaiah 14:28-32

28Neno hili lilikuja mwaka ule Mfalme Ahazi alipofariki:
29 aMsifurahi, enyi Wafilisti wote,
kwamba fimbo iliyowapiga imevunjika;
kutoka mzizi wa huyo nyoka
atachipuka nyoka mwenye sumu kali,
uzao wake utakuwa joka lirukalo,
lenye sumu kali.

30 bMaskini kuliko maskini wote watapata malisho,
nao wahitaji watalala salama.
Lakini mzizi wako nitauangamiza kwa njaa,
nayo njaa itawaua walionusurika.


31 cPiga yowe, ee lango! Bweka, ee mji!
Yeyukeni, enyi Wafilisti wote!
Wingu la moshi linakuja toka kaskazini,
wala hakuna atakayechelewa katika safu zake.

32 dNi jibu gani litakalotolewa
kwa wajumbe wa taifa hilo?
Bwana ameifanya imara Sayuni,
nako ndani yake watu wake walioonewa watapata kimbilio.”
Copyright information for SwhKC